Sisi ni nani

Shirika la Mozilla linafanya kazi ili kuhakikisha kuwa mtandao unabaki kuwa rasilimali ya umma iliyo wazi na ambayo sisi sote tunaweza kuifikia.

Mwanzoni mwa miaka ya 2000, jamii ya Mozilla ilitengeneza Firefox. Tuliondoa ukiritimba wa kivinjari, tukawapa watumiaji chaguo na udhibiti mtandaoni, na tukasaidia kuunda maadili mema ya mtandao.

Miaka ishirini baadaye, Mozilla inaendelea kupigania maadili mema ya mtandao — ambapo Makampuni makubwa ya kimataifa ya teknolojia yanawajibika na watumiaji binafsi wana wakala wa kweli mtandaoni.

Kazi ya Mozilla inaongozwa na Hati ya kutangaza kanuni ya Mozilla. Ilianzishwa kama mradi wa jumuiya huria mnamo 1998, Mozilla kwa sasa ina mashirika mawili: 501(c)3 Mozilla Foundation, inayoongoza kazi yetu ya ujenzi; na tanzu yake inayomilikiwa kabisa, Shirika la Mozilla, linaloongoza kazi yetu ya msingi wa soko. Mashirika haya mawili yanashirikiana na jumuiya ya kimataifa ya maelfu ya watu wanaojitolea chini ya bendera moja: Mozilla.

Mtandao wa intaneti ni rasilimali ya umma ya kimataifa ambayo lazima watu wote waweze kuufikia.

Hati ya kutangaza kanuni ya Mozilla

Dhamira yetu

Leo mtandao wa intaneti upo kila mahali. Inaunda uchumi, inashawishi serikali, na ni muhimu kwa mabilioni ya maisha. Lakini sisi ndio tutaamua ikiwa mtandao utakuza demokrasia, soko huria, na uhuru wa kujieleza au ubaguzi, ufuatiliaji wa watu wengi, na habari potofu.

Ni wajibu wa Mozilla kuhakikisha kuwa mtandao unabaki kuwa zana nzuri.

Kwa zaidi ya miongo miwili, Mozilla imewekeza katika mawazo ya ujasiri, viongozi wa kimataifa, na kampeni za kiraia. Tunafanya kazi katika mipaka, nyanja, na teknolojia ili kudumisha kanuni kama vile faragha, ujumuishaji na ugatuzi mtandaoni. Mbinu zetu ni tofauti, lakini maono yetu ni moja: harakati thabiti kwa ajili ya maadili mema ya mtandao.

Mnamo 2019, tuligundua changamoto mpya katika maadili mema ya mtandao: akili ya bandia. AI inatufanyia maamuzi na inafanya maamuzi kuhusu mambo yanayotuhusu, lakini siyo kila wakati. Inaweza kutuambia habari tunazosoma, matangazo tunayoona, au ikiwa tunastahiki kupata mkopo.

Maamuzi ambayo AI hufanya yanaweza kusaidia wanadamu, lakini pia yanaweza kutudhuru. AI inaweza kukuza upendeleo wa kihistoria na ubaguzi. Inaweza kutanguliza ushiriki badala ya ustawi wa mtumiaji. Inaweza kuimarisha zaidi uwezo wa Makampuni makubwa ya kimataifa ya teknolojia na kuwatenga watu binafsi.

Mozilla ipo katika nafasi ya kipekee ya kukabiliana na changamoto hii. Maadili yetu ya msingi ni uwazi na ujumuishaji. Historia yetu imejaa mawazo kabambe na utetezi uliofanikiwa mtandaoni.

Wakati ambapo tunahitaji sana AI ya kuaminika, Mozilla inaweza kusaidia.

Jihusishe

Jiunge nasi na usaidie kulinda mtandao kama rasilimali ya umma ya kimataifa. Ili kuanza, chunguza fursa za kushiriki au utoe mchango.

Fanya kazi nasi

Hapa Mozilla, tunawahudumia binadamu — kwa kudumisha intaneti salama, ambayo watu wote wanaweza kufikia — huku pia tukiwasaidia wanadamu walioajiriwa hapa kufikia malengo yao binafsi na ya kitaaluma.

Nafasi za kazi za Mozilla Foundation →

Shirikiana nasi

Toa mchango kwa kufadhili, kuunda, na kuendeleza kazi ya Mozilla ya kuhakikisha mtandao mzuri ulio na faragha, uwazi na ushirikishwaji na uwezo wa akili bandia unaoaminika.

Tushirikiane →